Askofu mkuu wa kanisa la Angrikana nchini Mhashamu Jacobu Chimeledya
amewatadhariwa waumini na watanzania kwa ujumla kutambua kuwa amani
iliyopo inaweza kuendelea kumomonyoka na kuwa vurugu, kama hawatakuwa
tayari kutoa taarifa kwa vyombo vya dora, juu ya watu wachache ambao
wanajihusisha na utengenezaji wa milipuko.
Mhashamu Chimeledya ametoa kauri hiyo katika maubiri yake katika kanisa
la angrikana mjini Tabora, katika maazimisho ya miaka 25 ya dayosisi ya
Tabora, ambapo amesema kuwa, matukio ya milipuko yanayojitokeza katika
baadhi ya mikoa wahusika wamo katika jamii, ambayo kama ikishirikiana
yanaweza kutolewa taarifa.
Wakizungumzia misingi ya amani iliyopo ndani ya kanisa na taifa zima, baadhi ya viongozi wa makanisa mbalimbali wamesema kuwa, jamii ibadilike kwa kutambua amani ikitoweka waathirika wakubwa ni watanzania wote, na hakuna pakukimbilia.
Dayosisi ya Tabora imeazimisha miaka ishirini na tano kwa matukio mbalimbali ikiwemo shughuli za kimaendeleo kama kuanzishwa kwa shule za sekondari, na vituo vya afya, likiwa na lengo la kutoa mchango kwa serikali katika huduma za kijamii katika kuleta maisha bora kwa kila mtanzania.
Wakizungumzia misingi ya amani iliyopo ndani ya kanisa na taifa zima, baadhi ya viongozi wa makanisa mbalimbali wamesema kuwa, jamii ibadilike kwa kutambua amani ikitoweka waathirika wakubwa ni watanzania wote, na hakuna pakukimbilia.
Dayosisi ya Tabora imeazimisha miaka ishirini na tano kwa matukio mbalimbali ikiwemo shughuli za kimaendeleo kama kuanzishwa kwa shule za sekondari, na vituo vya afya, likiwa na lengo la kutoa mchango kwa serikali katika huduma za kijamii katika kuleta maisha bora kwa kila mtanzania.
0 comments:
Chapisha Maoni