Serikali
 ya CHINA imekabidhi msaada wa gari la kisasa la kurushia matangazo ya 
nje ya televisheni kwa Shirika la Utangazaji TANZANIA, TBC, lenye 
thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni SITA.
 Akizungumza katika 
hafla ya uzinduzi wa gari hilo jijini DSM, Makamu wa Rais wa CHINA, LI 
YUCHUAN amesema msaada huo unalenga kudumisha uhusiano mwema kati ya 
nchi hizo mbili na kuongeza kuwa serikali yake inaamini kuwa utatumika 
kuwaunganisha Wachina na Watanzania kupitia vipindi mbalimbali katika 
Nyanja za Uchumi, Elimu, Sayansi, Teknolojia na Utamaduni.




0 comments:
Chapisha Maoni