Mr Blue aka Kabayser ambaye kwa mwaka huu (2014) hajatoa wimbo mpya
baada ya ‘Pesa’ iliyotoka mwishoni mwa mwaka jana, amesema anatambua
kuwa ana deni kubwa linalomuumiza kichwa analodaiwa na mashabiki wake na
yuko tayari kulilipa siku si nyingi.
“Mwaka huu bwana nafanya video, inaniumiza kichwa kwasababu muda
mrefu nadaiwa video na mashabiki”, alisema Kabayser leo.
Blue ambaye ana muda mrefu hajatoa video ya wimbo wake amesema
anatarajia kufanya video ya ‘Pesa’ na atafanya na Adam Juma. “ndani ya
mwezi huu (April) kwasababu nilishamalizana na Adam nasikilizia anipe
tarehe niweze kupiga kazi”.
Baada ya video ya ‘Pesa’ kukamilika na kutoka mwezi ujao (May), Blue
amesema atatoa wimbo wa crew yake ya Micharazo kabla ya kufikiria
kutoa single yake mwenyewe mpya.



0 comments:
Chapisha Maoni