Jumatano, Aprili 09, 2014

MATUKIO MAKUBWA YALIYOTOKEA DUNIANI SIKU KAMA YA LEO APRIL 9 MIAKA TOFAUTI ILIYOPITA

Siku kama ya leo miaka 8 iliyopita, inayosadifiana na tarehe 20 Farvardin 1385 Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilifanikiwa kupata teknolojia ya kurutubisha madini ya urani kwa ajili ya matumizi ya kiraia. Wasomi na wataalamu wa Iran walifanikiwa kukamilisha mfumo wa kuzalisha nishati ya nyuklia licha ya mbinyo na vikwazo vya nchi za kibeberu. Kwa utaratibu huo Iran iliingia katika kundi la nchi zenye teknolojia ya nyuklia duniani. Mwaka mmoja baadaye Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilianza kuzalisha nishati hiyo viwandani. Mafanikio hayo makubwa ya Iran yalipatikana chini ya usimamizi wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA). Hata hivyo baadhi ya nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani zinapinga vikali miradi ya nishati ya nyuklia ya Iran kutokana na sera zao za kindumakuwili na za kibaguzi.

Tarehe 9 Aprili miaka 11 iliyopita, mji mkuu wa Iraq Baghdad ulitekwa na majeshi ya Marekani na waitifaki wake na utawala wa Saddam Hussein ukasambaratika. Marekani ilianza kuishambulia Iraq tarehe 20 Machi mwaka 2003 na ilitazamiwa kwamba jeshi hilo vamizi lingekabiliwa na upinzani mkali wa majeshi ya Iraq mjini Baghdad. Lakini la kushangaza ni kuwa askari wa Marekani waliingia mjini humo bila ya kukabiliwa na upinzani mkali. Tangu wakati huo Washington imekuwa ikipora utajiri wa Iraq hususan maliasili ya mafuta ya nchi hiyo na kufanya jitihada zaidi za kudhibiti nchi nyingine za Mashariki ya Kati.

Na siku kama ya leo miaka 66 iliyopita utawala ghasibu wa Israel ulifanya mauaji ya kinyama katika kijiji cha Deir Yassin huko magharibi mwa Baitul Muqaddas. Mauaji hayo yalifanyika wakati wa vita vya kwanza vya Waarabu na Israel na yalitekelezwa na Wazayuni wa kundi la Irgun lililokuwa likiongozwa na waziri mkuu wa zamani wa Israel Menachem Begin. Eneo la Dier Yassin lilikuwa na umuhimu mkubwa kwa Wazayuni kutokana na kuwa katika njia ya Baitul Muqaddas na karibu na pwani. Baada ya kukivamia kijiji cha Deir Yassin, Wazayuni hao waliwaua kinyama wakazi 270 ambao hawakuwa na hatia yoyote wa kijiji hicho. Mauaji hayo yaliwalazimisha Wapalestina wengi wa eneo hilo kukimbia makazi yao kwa kuhofia kukaririwa mauaji kama hayo ya kinyama.

0 comments:

Chapisha Maoni