STAA wa Bongo Fleva, Isabela Mpanda amewachana wasanii ‘wanaotembea’ na
mameneja wao kwani ni ujinga wa mawazo na yeye kamwe hawezi kufanya
hivyo.
Akizungumza na mtandao huu hili, Isabela alisema katika maisha yake
hajawahi kuwa na uhusiano na meneja au prodyuza na huwa anawashangaa na
kuwasikitikia wasanii wanaofanya hivyo wakati siyo njia sahihi ya
kujikwamua kimuziki.
“Huwezi kuchanganya kazi na mapenzi, kamwe siwezi kutoka kimapenzi na
meneja wangu kwa sababu najua ufanisi wa kazi utakuwa mdogo tu,”
alisema Isabela.
0 comments:
Chapisha Maoni