Mpaka sasa mtoto huyo ana miaka tisa, lakini mchezo huo umekuwa
sehemu ya maisha yake na kuathiri hata uwezo wake darasani. Endelea
kujua kilichofuata.
Baada ya kukagua daftari za mtoto huyo na kuona
hesabu ambazo haziendani na mwanafunzi wa darasa la pili, bibi Lebai
alilazimika kwenda shule kwa lengo la kuzungumza na walimu kujua
inakuwaje.
Anasema alipofika shuleni na kukutana na mwalimu
wa mtoto huyo akagundua kuwa hesabu hizo hazikuwa zikifundishwa darasani
wala kusahihishwa na mwalimu kama alivyokuwa akidhani.
Anaeleza kuwa baada ya kuona daftari kwa haraka
mwalimu akagundua mwandiko huo ulikuwa wa mwanafunzi wa kiume wa darasa
la nne ambaye alimtaja kwa jina.
“Mwalimu alivyoangalia tu akasema huu ni muandiko
wa kijana fulani wa darasa la nne, nadhani alikuwa anamuandikia na
kumsahihishia muda wanaokutana na alikuwa anafanya hivyo ili nisipate la
kumuuliza maana alikuwa akipata hesabu zote,” anasema.
Jambo hilo lilimkwaza na kuona kuwa mtoto huyo
hawezi kubadilika akiwa shuleni hapo, akalazimika kumhamishia kwa
shangazi yake ambako alihisi huenda mazingira mapya yangembadilisha
tabia.
Anasema akafanya taratibu zote na kumhamishia
katika shule ya msingi Kunguru iliyopo Tegeta Mbuyuni, lakini huko ndiko
hali ilipozidi kuwa mbaya zaidi kwani alikuwa akitumia muda mrefu
kushinda porini kufanya mchezo huo na wanafunzi wenzake.
“Nikajua kule atakuwa mgeni huenda ndiyo ingekuwa
mwisho wa mchezo wake kumbe kule ndiyo ilikuwa balaa kuna pori moja
ambalo ndiyo limekuwa sehemu yake anawachukua wanafunzi wenzie na kwenda
nao huko,” anasema na kuongeza:
“Nikaanza kupata malalamiko kutoka kwa shangazi
yake kuwa anachelewa mno kurudi, na hata akirudi anakuwa amechafuka
kiasi kwamba ni ngumu kuamini kuwa alikuwa shuleni”.
Anasema akajaribu kuanza tena kumchunguza mwenendo
wake na kugundua kuwa huwa haandiki, na hata anapoandika daftari zake
hazisahishwi na walimu.
“Mwenendo wake wa kuchelewa kurudi ulinifanya
nianze tena kumchunguza kwa undani nikawa naangalia daftari zake,
nikaona ameanza uvivu wake wa kutoandika na kusahishiwa daftari
nikalazimika kwenda tena shuleni kujua maendeleo yake,” anasema.
Anasema alipofika na kujitambulisha kwamba ni bibi
wa mtoto huyo walimu walimshangaa na kumuelezea kuwa hawakuwa
wakiuelewa mwenendo wake kutokana na muonekano wake kuhisi kuwa huenda
ana matatizo ya akili.
“Walimu wake walinishangaa wakaniambia kila siku wanamwambia amlete mzazi wake ila akawa anawazungusha, wakasema pia kuwa shule huwa anafika lakini haandiki,” anasema.
“Walimu wake walinishangaa wakaniambia kila siku wanamwambia amlete mzazi wake ila akawa anawazungusha, wakasema pia kuwa shule huwa anafika lakini haandiki,” anasema.
Walimu wakambana ili aseme mahali anaposhinda muda
ambao wenzake wanakuwa darasani, bakora alizochapwa na mwalimu wake
zilimsukuma kuwataja wote ambao waliwahi kumuingilia.
Anasema alitaja orodha ndefu ya watu ambao
wamewahi kumuingilia kimwili wakiwamo wanafunzi wenzake pamoja na vijana
wengine ambao wanaonekana kuwa na umri unaokadiriwa kufikia miaka 30.
“Akaandika majina hayo mwenyewe kwenye karatasi,
binafsi nikaona ili kumuepusha na dhahama hiyo ni bora akae nyumbani
asiende shule maana huo ndiyo upenyo anaoutumia kufanya mchezo wake.
“Lakini kila ninapofikiria umuhimu wa elimu naona
nitamkosesha huyu mtoto kupata haki yake ya msingi, ndiyo maana naomba
msaada aweze kupata shule ya bweni ya wasichana tupu ambayo pia itakuwa
na misingi ya dini huenda akabadilika na kuwa kama watoto wengine,”
anasema.
Anasema pamoja na suala la shule huenda mtoto huyu
anahitaji matibabu kwa kuwa tabia hiyo inaonekana kuathiri akili yake
kiasi kwamba hata muda anaokuwa mwenyewe anadiriki kuchana nguo zake za
ndani.
“Ukiangali nguo zake za ndani karibu zote katikati
zina matobo anatoboa ili awe anajiingiza vidole,wakati mwingine hata
akilala na watoto wenzake wanalalamika anapenda kuwapapasa kitu ambacho
nahisi hata kwenye akili yake hatakuwa sawa,” anasema.
Baada ya kupata maelezo hayo ya bibi Lebai,
mwandishi wa makala haya alifanya jitihada za kumpeleka mtoto huyo
hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na kujua hali yake ya afya
kwa ujumla.
Vipimo vilichukuliwa na Dk. Rose Mbeyele wa
Hospitali ya Rufaa ya Amana ambaye alithibitisha mtoto huyo kuingiliwa
kimwili sehemu zake za siri mbele na nyuma.
Jambo la kushukuru majibu ya damu na mkojo
hayakuonyesha mtoto huyo kuwa na tatizo lolote kiafya wala dalili za
kunyemelewa na ugonjwa wowote wa zinaa kwa wakati huo.
Hata hivyo mwandishi wa makala alifanya jitihada za kumtafuta mama wa mtoto huyo, kujua sababu ya kuruhusu mtoto wake afanyiwe ukatili wa aina hii tena angali akiwa mdogo mpaka sasa tatizo linazidi kuwa sugu.
Hata hivyo mwandishi wa makala alifanya jitihada za kumtafuta mama wa mtoto huyo, kujua sababu ya kuruhusu mtoto wake afanyiwe ukatili wa aina hii tena angali akiwa mdogo mpaka sasa tatizo linazidi kuwa sugu.
Mwanamke huyo anayejitambulisha Julieth Anthony
anasema ugumu wa maisha ulimfanya kushindwa kuishi na watoto wake
wawili, hivyo kushindwa kushiriki kikamilifu katika malezi.
Anasema tangu amzae mtoto huyu hajapata fursa ya
kukaa naye kwa muda mrefu ili kujua tabia na mwenendo wake wa kila siku
na hilo linasababishwa na ugumu wa maisha, kutokana na kukosa shughuli
maalumu ya kufanya.
Hata hivyo Julieth anakiri kuwa mtoto wake alianza
kuharibika wakati yuko naye kutokana na mihangaiko aliyokuwa nayo, hali
iliyokuwa ikimsababishia mara kwa mara kumuacha mtoto huyo peke yake.
“Katika harakati za kujitafutia riziki nilikuwa
naamka asubuhi na kwenda kuuza chapati mbali kidogo na nyumbani nikiwa
nimemuacha mtoto kumbe wakati huo ndiyo alikuwa akifanyiwa mchezo huo na
mtoto wa mpangaji mwenzangu.
“Bibi yake alipokuja kumchukua ndiye aliyemhoji na
kujua hilo kiukweli kama mama niliumia lakini sikuwa na namna ya
kufanya, kwa sasa binafsi sijui kama anaendelea au ameacha kwa kuwa
sijapata fursa ya kuishi naye tangu alipochukuliwa akiwa na miaka
miwili,” anasema.
Kuhusiana na kushindwa kutimiza wajibu wake kama
mama kwa mtoto huyo anasema hilo lilitokana na kutengana na baba wa
mtoto huyo baada ya kuzaliwa hali iliyomsababishia watoto wake wawili
kulelewa na bibi yao.
Anasema kwa muda mefu kumekuwa na hali ya
kutoelewana kati yake na ndugu wa mzazi mwenzake akiwamo bibi anayemlea
mtoto huyo hivyo kushindwa kabisa kujua maendeleo yake.
“Sina kazi wala biashara maisha yangu ni ya
kubaingiza vilevile sina maelewano mazuri na mama mkwe wangu, hali
inayosababisha mimi kushindwa kumlea mwanangu na matokea yake
anajihusisha kwenye tabia za ajabu napatwa na uchungu sana kama mama,
lakini sina cha kufanya hiyo yote kwa sababu ya umaskini,” anasema.
Nipeni huyo mtoto mimi.Sidhani kama an shida kubwa kiasi hicho. Hakuna kinaweza kushindikana. Atafika mbali sana kimasomo. Niko Moshi.
JibuFuta