NI madai mazito! Kwamba, nyota wa muvi za Kibongo, Kajala Masanja amehongwa gari na mtu anayedaiwa kuwa ni kigogo wa Ikulu.
Kwa mujibu wa habari hizo ambazo zipo hadi kwenye mitandao ya kijamii,
hasa Instagram, Kajala alinunuliwa gari hilo aina ya Toyota Brevis lenye
rangi ya bluu iliyoiva wiki mbili zilizopita mara baada ya kutua Bongo
akitokea nchini China ambako alikwenda kwa mambo yake binafsi.
Wasambaza taarifa hao walidai kuwa, kigogo huyo wa Ikulu ni yule
Clement ambaye amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi wa Miss Tanzania
2006, Wema Sepetu.
“Mmeisikia hii? Kajala amenunuliwa gari na Kile (Clement), lina
thamani ya shilingi milioni kumi na moja, Wema alie tu nakwambia. We
ukisema cha nini wenzako wanajiuliza watakipata lini?
![]() |
KAJALA MASANJA |
“Kwanza mnajua kama bifu la Wema na Kajala lilitokana na Clement?
Alipoachana na Wema akatua kwa msichana anaitwa Naima, lakini akaona
bado akaenda hadi kwa Kajala. Wema alipogundua ndiyo akamnunia na kuanza
ushoga na Aunt Ezekiel,”Kilidai chanzo.
![]() |
GARI ALILONUNULIWA KAJALA |
Awali, mtoa habari mmoja alisema Kajala yupo na gari hilo Kinondoni kwa Manyanya, lakini alipofuatwa hapo hakuonekana.
Habari zikapatikana kwamba, alikuwa kwenye Mgahawa wa Steers uliopo jengo la Millennium Tower, lakini pia alipofuatwa eneo hilo hakuonekana.
Habari zikapatikana kwamba, alikuwa kwenye Mgahawa wa Steers uliopo jengo la Millennium Tower, lakini pia alipofuatwa eneo hilo hakuonekana.
Kuhusu kufa kwa ushoga wao, awali Kajala hakutaka kulizungumzia suala
hilo lakini alipobanwa alidai hana tatizo na Wema na kwamba kwa sasa
yuko bize kutengeneza filamu zake.
Kwa upande wake, Wema alipopigiwa simu hakupokea lakini siku za nyuma
aliwahi kuanika kwamba haamini kama Kajala anaweza kutembea na Clement.
Hapo ni wakati ule wakiwa mashoga.
0 comments:
Chapisha Maoni