Ijumaa, Januari 24, 2014

TAARIFA YA FEDHA WILAYA YA MBOZI YAMPA MSHITUKO ABBAS KANDORO

kuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro aikataa taarifa ya matumizi ya fedha zaidi ya Sh174 milioni za miradi miwili ya bwawa la maji katika Kijiji cha Iyula na Msia wilayani hapa na kutoa wiki moja kwa halmashauri ya wilaya kutoa maelezo sahihi ya miradi hiyo.

Katika fedha hizo,Sh134 milioni zimetumika katika Mradi wa Bwawa la Maji katika Kijiji cha Iyula huku fedha zilizopokelewa kutoka serikalini zikiwa Sh250 milioni na nyingine ni Sh40 milioni za Mradi wa Bwawa la Kijiji cha Msia ambapo fedha hizo zimetumika huku mradi ukiwa bado haujaanza kutekelezwa.
Alipotembelea miradi hiyo, Kandoro alisema, katika Mradi wa Bwawa la Iyula taarifa ya mkaguzi inaonyesha, fedha zilizopokelewa ni Sh250 milioni na zilizotumika ni Sh134 milioni. “Fedha zingine zimekwenda wapi kwani akaunti ya kijiji zilitolewa fedha zote Sh250 milioni na mbaya zaidi mmeomba fedha zingine nahitaji maelezo sikubaliani na taarifa yenu,”alisema Kandoro.
Kuhusu mradi wa Bwawa la Msia, Kandoro alisema hakubaliani na taarifa ya matumizi ya fedha hizo ambazo ni Sh40 milioni kwani hakuna kazi iliyofanyika zaidi ya michoro, utafiti na semina.
Alisema Serikali ya mkoa haiwezi kukubali kuona fedha za miradi ya maendeleo ya wananchi zinatumika vibaya na yeyote atakaye bainika kuhusika na ubadhilifu wa fedha hizo, ikiwa ni pamoja na kubadilisha matumizi yaliyokusudiwa atachukuliwa hatua kali za kisheria.
“Fedha nyingi za Serikali zinaletwa huku lakini hazitumiki kama ilivyokusudiwa,”alisema
Mwenyekiti wa Kamati ya Mradi wa Bwawa la Iyula, Jua Mwamlima alisema, walipokea fedha katika akaunti ya kijiji Sh250 milioni na fedha hizo zilitolewa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza zilitolewa Sh115 milioni na awamu ya pili zilitolewa Sh134 milioni.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Mradi wa Bwawa la Msia,Godwell alisema kuwa,fedha hizo walizitumia kwa ajili ya semina,kuwalipa waliofanya utafiti na wataalamu wa michoro .
Mkuu wa Wilaya ya Mbozi,Dk Michael Kadeghe alisema atahakikisha anasimamia maagizo hayo.

0 comments:

Chapisha Maoni