Alhamisi, Januari 23, 2014

MAKUBALIANO YA ADDIS ABABA YATIWA SAINI, VITA KISHA SUDAN YA KUSINI NDANI YA MASAA 24

Serikali ya Sudan Kusini na waasi nchini humo wametia saini makubaliano ya kusitisha mapigano katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa.
Machafuko ya ndani nchini Sudan Kusini yamesababisha vifo vya maelfu ya watu katika nchi hiyo changa zaidi duniani.

Wawakilishi wa Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini na kiongozi wa waasi Riek Machar walitia saini makubaliano hayo jana chini ya upatanishi wa jumuiya ya IGAD. Makubaliano hayo yanasisitiza kuwa mapigano nchini Sudan Kusini yanapaswa kusitishwa katika kipindi cha masaa 24.
Wapatanishi katika mzozo huo wamesema makubaliano hayo yataweka utaratibu wa kusimamia usitisha mapigano na kuruhusiwa shughuli za wafanyakazi wa operesheni za misaada ya kibinadamu.
Mapigano ya ndani nchini Sudan Kusini kati ya jeshi la serikali na waasi wanaoongozwa na makamu wa zamani wa rais Riek Machar yalianza tarehe 15 Disemba mwaka 2013. Baadaye mapigano hayo yalichukua sura ya kikabila baina ya kabila la Dinka la Rais Kiir na lile na Noer na Machar.

0 comments:

Chapisha Maoni