Ijumaa, Desemba 13, 2013

MASHINDANO YA MISS UTALII YAFUNGIWA, KAMA HUJAPATA TAARIFA HII..SOMA HAPA

Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) limefungia mashindano ya Miss Utalii Tanzania kwa muda usiojulikana kuanzia Oktoba 10, 2013.
Akitangaza taarifa hiyo kwa niaba ya Kaimu Katibu Mtendaji, Ofisa Habari Mkuu wa Basata, Agnes Kimwaga alisema uamuzi huo umetokana na waandaaji wa mashindano hayo kukiuka masharti, kanuni miongozo na taratibu za uendeshaji mashindano ya urembo kama ilivyowekwa na Serikali.
Alisema pia waandaaji hao walishidwa kufanya tathimini ya mashindano ya Misis Utalii 2012/13 kwa muda uliokubalika baada ya mashindano pamoja na Basata kuwakumbusha kufanya hivyo.
“Uamuzi huu umefikiwa baada ya kupatikana kwa ushahidi wa kutosha kutoka kwa warembo wenyewe juu ya unyanyaswaji wa kijinsia kwa washiriki, ikiwemo wale waliojihusisha kimapenzi na viongozi wa juu wa mashindano ili kupewa ushindi,” alidai Agnes.
Akizungumzia suala hilo, Rais wa Miss Utalii Tanzania, Gideon Chipengaulo alisema ni kweli wamepokea uamuzi wa Basata lakini sababu walizoelezwa kusimamishwa ni kuweka kambi kwa muda mrefu, kutokukamilisha tathimini kwa wakati na kuhamisha sehemu ya mashindano.
Alisema uamuzi huo wa Basata hauichukulii kama adhabu, kwani Bodi ya Miss Utalii Tanzania ilishaamua kusimamisha mashindano hayo kwa msimu wa mwaka mmoja tangu Agosti 2013 baada ya kugundua kasoro mbalimbali ikiwemo hujuma kutoka kwa baadhi ya wajumbe na washiriki.
“Katika kipindi cha miaka mitano tuliyoendesha mashindano, kumekuwepo na hujuma nyingi ikiwemo kupandikizwa kwa washiriki na baadhi ya wajumbe wa bodi waliokuwa na lengo la kuharibu mashindano,” alidai Chipungahelo.

0 comments:

Chapisha Maoni