Alhamisi, Novemba 07, 2013

MATUKIO MAKUBWA YANAYOKUMBUKWA LEO NOVEMBA 7

Miaka 146 iliyopita katika siku kama ya leo Madam Escudo Doska ambaye baadaye alikuwa maarufu kwa jina la Marie Curie alizaliwa huko Warsaw mji mkuu wa Poland. 
Baba yake alikuwa profesa wa fizikia na baadaye Madam Curie pia alielekea Paris Ufaransa kwa ajili ya kuendeleza masomo yake katika taaluma hiyo hiyo kama alivyofanya baba yake.
Hatimaye mwanamama huyo alifanikiwa kuvumbua mada ya radium baada ya utafiti na kutwalii kwa miaka mingi. Ni vyema kuashiria hapa kuwa Madam Curie alitunukiwa tuzo ya Nobel mara mbili katika taaluma za fizikia na kemia na aliaga dunia mwaka 1934.

Na siku kama ya leo miaka 57 iliyopita vita vya mfereji wa Suez vilimazika baada ya Umoja wa Mataifa kuingilia kati. Vita hivyo vilianza baada ya wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel kushambulia jangwa la Sinai na kufuatia mashambulizi ya askari wa miavuli wa Uingereza na Ufaransa katika eneo la mfereji huo.
Serikali hizo tatu zilianzisha vita hivyo kufuatia hatua ya rais wa wakati huo wa Misri Gamal Abdulnassir ya kuutaifisha mfereji wa Suez.

0 comments:

Chapisha Maoni