Jumatatu, Novemba 04, 2013

MATUKIO MAKUBWA MATATU YANAYOKUMBUKWA ZAIDI DUNIANI LEO NOVEMBER 4

Leo ni Jumatatu tarehe 29 Mfungo Tatu Dhulhija mwaka 1434 Hijiria, inayosadifiana na tarehe 4 Novemba mwaka 2013 Miladia.
Siku kama ya leo miaka 49 iliyopita, askari vibaraka wa utawala wa Shah uliokuwa ukitawala nchini Iran waliivamia nyumba ya Imam Khomeini muasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Qum na kumtia mbaroni. Baada ya kumhamishia mjini Tehran utawala wa Shah ulimbaidishia Imam Khomeini nchini Uturuki. Utawala wa Shah uliamua kufanya hivyo kutokana na uungaji mkono wake kwa harakati za mapambano za wananchi wa Iran za kutaka kuung'oa madarakani utawala huo. Lengo la kumbaidisha kiongozi huyo wa kidini, kisiasa na mwanamapinduzi, lilikuwa ni kusimamisha harakati za kiongozi huyo pamoja na mapambano ya wananchi Waislamu wa Iran dhidi ya utawala huo.


Siku kama ya leo miaka 67 iliyopita, Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO, liliasisiwa kwa ushirikiano wa nchi 43. Lengo la kuasisiwa taasisi hiyo lilikuwa ni kuanzisha mawasiliano ya kielimu na kiutamaduni baina ya mataifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusambaza vitabu na makala kwa lugha mbalimbali duniani. Miongoni mwa nukta muhimu za kuvutia zilizoko katika hati ya UNESCO ni haja ya watu wote kuheshimu uadilifu, utawala wa sheria na kulinda haki za binadamu pamoja na uhuru wa mwanadamu. Katibu Mkuu, Kamati ya Utendaji na Vikao vya Baraza Kuu ndizo nguzo muhimu tatu za kimsingi za Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa.

Na miaka 18 iliyopita kama leo, Is'haq Rabin Waziri Mkuu wa zamani wa utawala wa Kizayuni wa Israel aliuawa na Mzayuni mwenye misimamo ya kufurutu ada. Is'haq Rabin alifanikiwa kuwa Waziri Mkuu wa Israel kuanzia mwaka 1974 hadi 1977 kwa tiketi ya Chama cha Leba. Hata hivyo aliuzuliwa wadhifa huo kwa tuhuma za ubadhirifu. Ni muhimu kukumbusha kuwa, Is'haq Rabin alikuwa mingoni mwa makamanda wa makundi ya kigaidi ya Kizayuni.

0 comments:

Chapisha Maoni