Alhamisi, Oktoba 24, 2013

HII NDIO SABABU YA KUANZISHWA KWA OPARESHENI KIMBUNGA TANZANIA

Kiongozi wa Timu ya Habari na Mawasiliano ya Operesheni Kimbunga, Zamaradi Kawawa amesema opereshani hiyo haijaundwa kwa lengo la kumuonea yeyote wala kuwaondoa watu wa taifa fulani, bali kujua nani anaishi kwa haki na nani haishi kwa kufuata haki.
Anasema mpaka kufikia Septemba 20, 2013, wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 9,283 toka nchi za Rwanda, Burundi, Uganda, Somalia, DRC Congo, Yemen na India, kwa madai ya kuishi nchini isivyo halali.
Zamaradi anasema kilichomsukuma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete kuanzisha operesheni hiyo ni kukithiri kwa matukio ya uhalifu hasa katika mikoa iliyopo pembezoni mwa nchi.
“Operesheni Kimbunga ilianzishwa kwa lengo la kukabiliana na vitendo vya uhalifu vilivyokithiri vikiwemo ujambazi wa kutumia silaha,ujangili, utekaji wa magari na mauaji ya kikatili pamoja na migogoro ya ardhi inayotokana na wafuagaji kutoka nchi jirani kuingiza mifugo yao kwa ajili ya malisho,” anasema Zamaradi.
Aidha amesema idadi kubwa ya wahamiaji haramu waliokamatwa ni kutoka Burundi (5,355) wakiafuatiwa na Rwanda (2,379), Uganda (939), DRC Congo (564), Somalia (44), Yemen (1) na India (1).

0 comments:

Chapisha Maoni