Jumatano, Agosti 28, 2013

MAJAMBAZI 9 MBARONI DAR

Jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar es salaam limewatia mbaroni majambazi tisa wa kutumia siraha akiwemo askari polisi wa kituo cha Kipolisi oysterbay jijin Dar es salaam.

Kamishna wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaamu Bw.suleimani Kova amesema majambazi hao wamekamatwa katika operesheni maalum ya jeshi hilo ambapo pia walifanikiwa kukamata sare za jeshi la wananchi Tanzania(JWTZ) zinazoaminika kutumika katika uhalifu pamoja na silaha na risasi Aidha kamanda kova ameeleza kukamata magari yanayosadikika kutumika katika uhalifu tofauti pamoja na yenye namba za usajili T865CEH aina ya carina,na T967 AUG carina.

0 comments:

Chapisha Maoni