HABARI KWA WAKATI KUTOKA HAPA

Tunakuhakikishia kupata habari zote zilizo muhimu kutoka ulimwenguni kote kwa wakati, unaweza kusubscribe mtandao wetu na ukawa unapokea habari zote katika email yako punde tu tuchapishapo machapisho yetu. Jiunge na mitandao yetu ya Facebook na Twitter kutupata kirahisi.

HABARI ZA MICHEZO

Sasa Fichuo tunakuhakikishia kupata taarifa zote za kimichezo kutoka viwanja mbalimbali duniani, lengo ni kuhakikisha hupitwi na lolote katika ulimwengu wa michezo.Jiunge na mitandao yetu ya Facebook na Twitter kutupata kirahisi.

TAARIFA ZA BURUDANI NA HABARI ZA WASANII

Unapenda masuala ya burudani? Ni jukumu letu kuhakikisha unazipata info zote za burudani na wasanii wanaokupa burudani, unapata video mpya, movie pamoja na muziki. Kaa karibu nasi.

KURASA ZA MAGAZETI KILA SIKU

Tunakupatia kila ambacho kinaandikwa katika magazeti ya Tanzania na nje ya Tanzania, usitie shaka ukishindwa kununua gazeti uipendalo, sogea karibu nasi na upate kila unachokihitaji.

MAHUSIANO

Fahamu mambo mengi katika ulimwengu wa mapenzi kwa kupitia dondoo, simulizi na visa mbalimbali kupitia Fichuo Online, Jiunge na mitandao yetu ya Facebook na Twitter kutupata kirahisi.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo UYOLE CULTURAL TOURISM. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo UYOLE CULTURAL TOURISM. Onyesha machapisho yote

Jumatatu, Januari 18, 2016

SEHEMU YA KUANGALIZIA BONDE LA UFA MBEYA (MBEYA RIFT VALLEY VIEWING POINT)

Mbeya ni kati ya mikoa ya Tanzania inayopitiwa na Bonde la ufa linalosadikika kutokea miaka 35 milioni iliyopita, bonde hili linatengeneza picha inayoonesha kuwa baada ya miaka kadhaa ijayo kupita, bara la Afrika litagawanyika kama ilivyo tokea miaka mingi iliyopita inayoaminika kuwa sayari ya dunia ilikua na bara moja lililojulikana kama PANGEA na kwa kutokana na mitikisiko iliyosababisha bara hilo kujigawa ikasababisha kutokea kwa mabara saba; hivyo basi tafiti za wana Jografia zinaonesha kuwa nchi za Afrika ya Mashariki zitajitenga/zitajigawa kutoka bara la Afrika na kutokea bara lingine.
Bonde hili la ufa limejigawa katika sehemu kuu ambazo ni: Upande wa Mashariki, Upande wa Magharibi na Upande wa Kusini
Upande wamashariki linaloanzia kuonekana katika nchi ya Syria (Magharibi mwa bara la Asia) kuelekea Kusini mpaka nyanda za juu Ethiopia, Somalia kuja Kenya kupitia ziwa Turkana; Mpakani na Tanzania kuna maziwa ya magadi kama Lake Natron. Ndani ya Tanzania baada ya kupita (mlima Kilimanjaro) bonde lapanuka hadi kutotambulika tena kwa macho. Kwenye (bonde la Usangu) linaonekana tena kama bonde lenye safu za milima kando.
La upande wa pili ni lile la Magharibi 
huonekana vizuri kuanzia ziwa Albertna kuendelea katika maziwa ya ziwa Edward, ziwa Kivu, ziwa Tanganyika na ziwa Rukwa.
Upande wa Kusini Kusini ya Mbeya ufa inaendelea katika Ziwa Nyasa, halafu katika mabonde ya mto Shire na sehemu ya mwisho wa mto Zambezi hadi kuingia katika Bahari Hindi.
Mbeya ni sehemu pekee ambapo pande zote za bonde la Ufa zinakutana (Mashariki, Magharibi na Kusini).
Pia unaweza kuliona kwa uzuri bonde hili kupitia maeneo mbalimbali ndani ya mkoa wa Mbeya, Lakini sehemu nzuri zaidi ni sehemu iitwayo RIFT VALLEY VIEWING POINT ambayo inapatikana katika eneo la misitu ya Kawetile barabara ya kuelekea Chunya, eneo hili ni zuri haswa kwa muonekano wake, hali ya hewa mwanana na linamuwezesha mtembeleaji kuona bonde la ufa kwa muonekano mzuri zaidi.
Pia eneo limetengenezwa vizuri kiasi kwamba linaweza kutumika katika kazi mbalimbali, kama kujifunza (study tour) sherehe tofauti tofauti kama Harusi na zingine, kupunga hewa, kupiga picha, kupumzika na zingine nyingi.
Ukitokea Mbeya mjini kuelekea eneo hilo utaweza kuona vitu mbalimbali kama; eneo maalum kwaajiri ya muonekano wa jiji (MBEYA CITY VIEWING POINT) katika sehemu hii utaweza kuiona sehemu kubwa ya jiji la mbeya, ukiendelea kupanda utaona Ofisi za hifadhi ya msitu wa Kawetile unaobeba historia kadhaa kama ukumbusho wa gereza la zamani, Barabara ya Uwanda wa Juu kuliko zote Tanzania yenye Altitude 2457M latitude 0835'S longitude 3325'E, Soko dogo la viungo (spice)na vyakula lililopo njiani, Kona kali sana iliyopewa jina la kona ya mkoa na vingine viingi saana na vizuri.
Nirahisi sana kuyafikia maeneo haya, wasiliana na UYOLE CULTURAL TOURISM ENTERPRISES, hawa watakuwa wenyeji wako katika kufurahia vivutio hivi hapa mkoani Mbeya,utawapata kwa simu 0783545464/0766422703.

Ijumaa, Januari 08, 2016

KATI YA VIVUTIO VILIVYOPO MKOANI MBEYA NI PAMOJA NA MAPOROMOKO YA MAJI MWALALO


Ni maporomoko yanayopatikana katika safu za milima ya LIVINGSTONE karibu na kingo za ziwa Nyasa (MATEMA BEACH), kijiji cha Matema, wilaya ya Kyela mkoani Mbeya. Mto huu humwaga maji yake ziwa Nyasa.

Maporomoko haya yapo sehemu ambayo ni nzuri kwa (ku hike) ambapo huchukua takribani saa 1 (1hr) kutembea kwa mwendo wa kawaida (kwa miguu) kutoka katika kijiji cha Matema.

Ni nzuri kutembelea eneo hilo kwa muda wa ziada pale unapotembelea fukwe za ziwa Nyasa kwaajili ya mapumziko au sababu za kitalii kwa ajili ya zoezi la mwili, moja kati ya interesting moment ni pale katika kakilima ka mwisho kanakohitaji kupanda kwa kujivuta katika kamba.

Eneo lina sifa ya muonekano mzuri hasa wa rangi nyeupe ya maji yanayoporomoka katika miamba ya rangi ya mvuto ya kijivu.

Maporomoko haya yametengeneza bwawa zuri na la asili katikati ya miamba (mawe) ambacho ni kizuri kwa kuogelea, na kupigia picha

Pia maporomoko ya Mwalalo ni eneo zuri kwaajiri ya kupigia picha kutokana na muonekano mzuri uliopo hapo (Ungependa video ya msanii gani ingerekodiwa hapo?) Tuthamini na kuvitangaza vivutio vyetu.
Kwa nini usimuliwe? Karibu sana UYOLE CULTURAL TOURISM ENTERPRISES ujionee kwa macho yako na ujifunze mengi na kuburudika uwapo maeneo haya.wasiliana nasi kwa simu 0783545464/0766422703.