Jumapili, Mei 22, 2016

FASTJET KUMLIPA MTANZANIA MILIONI 30 KAMA FIDIA

http://www.thetimes.co.uk/tto/multimedia/archive/00360/117474578_Fastjet_360622c.jpg
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeiamuru Kampuni ya Ndege ya Fastjet kumlipa abiria wake, John Mhozya fidia ya Sh30 milioni baada ya kushindwa kumtaarifu kuhusu kuahirishwa kwa safari yake.
Mbali na fidia hiyo ya hasara ya jumla aliyoipata abiria huyo kutokana na safari hiyo kufutwa, pia Mahakama hiyo imeiamuru kampuni hiyo kumrejeshea abiria huyo nauli yake ya Sh43,000 alizokuwa ameshalipa na Sh339,000 alizozitumia kwa nauli baada ya kutafuta usafiri mbadala kutoka shirika jingine la ndege.

0 comments:

Chapisha Maoni