Jumatatu, Januari 25, 2016

KWANINI UNASHAURIWA KUNYWA MAJI KIASI HIKI KABLA YA KULALA?

Kila mtu anajua umuhimu wa kunywa maji, lakini wanajua kunywa maji wakati wa mchana tu hawafahamu umuhimu wa kunywa maji wakati wa usiku, hasa kwa wazee wanaopata magonjwa ya mishipa ya damu kwenye moyo au ubongo.
Takwimu zinaonesha kuwa wazee wengi wanagunduliwa kupata kiharusi wakati wa asubuhi, wataalamu wanaona chanzo chake ni ukosefu wa maji wakati wa usiku. Ukosefu wa maji mwilini unaongeza uzito wa damu, na kusababisha magonjwa ya mishipa ya damu kwenye moyo na ubongo.
Wazee wengi hawapendi kwenda chooni wakati wa usiku, hivyo hawataki kunywa maji kabla ya kulala. Kutokana na kibofu cha mkojo kutofanya kazi vizuri, ukubwa wake unapungua, wingi wa mkojo unaongezeka na kusababisha ukosefu wa maji mwilini. Hivyo kunywa maji wakati wa usiku ni muhimu kwa wazee. Lakini kwa wazee wanao udhaifu wa moyo au upungufu wa uwezo wa moyo, hawafai kunywa maji mengi kabla ya kulala, ama sivyo shinikizo la damu litaongezeka.

CRI

0 comments:

Chapisha Maoni