Jumamosi, Januari 23, 2016

AJALI YA BM YAUA NA KUJERUHI MOROGORO

Taarifa kutoka mkoani Morogoro zilizofika katika meza yetu ya habari ya Fichuo, ni kuwa kuna ajali ya Basi la BM imetokea saa nne kasoro usiku.wa kuamkia leo maeneo ya Mikese Morogoro. 
Basi limegongana na gari lingine na kutumbukia kwenye Korongo. Taarifa tuliyoipata kutoka kwa chanzo chetu nikuwa kilichosababisha ajali ni mwendo kasi kwakuwa kuna gari lilikuwa limeharibika limeegeshwa pembeni. Kukawa kuna semi trailer inatoka Moro uelekeo DSM ikawa inalipita hilo gari lililoharibika, k
abla halijamalizika kulipita, BM ikawa imefika hapo ndio ikaingia katikati ya trailer.
Na taarifa zaidi kuhusu ajali hiyo ni kwamba watu wawili walipoteza maisha katika ajali hiyo huku wengine 43 wakijeruhiwa.


0 comments:

Chapisha Maoni