Jumatano, Oktoba 01, 2014

EBOLA YAVUKA BODA...SASA NDANI YA MAREKANI

Ugonjwa wa Ebola ambao umekuwa tishio kubwa duniani huku ikiripotiwa kusabisha vifo vingi katika eneo la Afrika Magharibi umeingia nchini Marekani ambapo mgonjwa wa kwanza ameripotiwa katika mji wa Dallas, Texas.
Mgonjwa huyo anaelezwa kuwa ni mtu aliyepata maambukizi alipokuwa nchini Liberia na aliingia Mareikani kabla ya kuonesha dalili za ugonjwa huo.
Maafisa wa kituo cha afya cha Texas katika hospitali ya Presbyterian wamesema kuwa mgonjwa huyo ambaye jina lake halikutajwa ametengwa katika hospitali hiyo.
Maafisa wa kitengo cha Afya cha Marekani wamewatoa hofu raia wa nchi hiyo wakisema wanaamini kuwa wataudhibiti ugonjwa huo kabla haujasambaa.
Shirika la Afya Duniani, WHO limesema mpaka sasa zaidi ya watu 3,000 wamekufa kutokana na virusi vya Ebola, wengi wa waliokufa ni kutoka Liberia.

0 comments:

Chapisha Maoni