Jumanne, Septemba 30, 2014

VYOMBO VYA HABARI VIMESHINDWA KUANDIKA KASHFA ZA RAIS WA ARGENTINA DHIDI YA MAREKANI

Vyombo vikuu vya habari duniani vimejizuia kurusha hewani matamshi ya Rais wa Argentina katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambayo yalikosoa vikali siasa za Marekani kimataifa.
Katika hotuba yake kwenye mkutano wa 69 wa Baraza Kuu, Bi. Cristina Fernandez de Kirchner Rais wa Argentina ameelezea masuala mbalimbali kuanzia mabadiliko yanayotakiwa kwenye Mfuko wa Fedha wa Kimataifa hadi matatizo ya Wapalestina na vita dhidi ya ugaidi.
Ameihoji Marekani kwamba imekuwaje sasa inashambulia baadhi ya makundi kama lile la kigaidi la Daesh ambalo imekuwa ikiliunga mkono ili liangushe serikali ya Syria.
Rais hiyo amekosoa siasa za alizoziita za ‘kindumilakuwili’ za Marekani, na kuuliza kwamba
Daesh na Al Qaeda wanapata wapi silaha? Jana walikuwa makundi ya ukombozi na leo ni magaidi?
Katika hatua nyiningine, rais huyo wa Argentina ametupilia mbali madai yanayotolewa dhidi ya Iran tangu mwaka 1994 kuhusiana na shambulizi la bomu lililolenga kituo cha Mayahudi mjini Buenos Aires, na kusema kwamba uchunguzi uliofanywa na na nchi yake umethibitisha kwamba Iran haikuhusika katika shambulio hilo.
Wapiganaji wa kudni la Daesh ambalo sasa ni kundi la kigaidi, mwaka 2012 lilipewa mafunzo na maajeti wa shirika la kijesusi la Marekani (CIA) huko nchini Jordan kwa lengo la kuiondoa madarakani serikali ya Syria.

0 comments:

Chapisha Maoni