Jumatatu, Septemba 01, 2014

UKWELI WA NDOA ILIYOVUNJIKA KANISANI DAR ES SALAAM

Katika hali isiyokuwa ya kawaida Paroko Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam Parokia ya Mtakatifu Yohane Mbatizaji Luhanga, Padri Richard D’souza, ameshindwa kufungisha ndoa baada ya bibi harusi kubainika kuwa ni mke wa mtu.
Bibi harusi aliyejulikana kwa jina la Neema Hoza, ambaye alitaka kufunga ndoa na mwanamme mwingine ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, anadaiwa kuwa alishafunga ndoa na Brighton Mhache katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Kimara.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, kaka wa mume wa Neema, Fadhili Mhache, alisema mdogo wake alikwishafunga ndoa na Neema, lakini cha kushangaza shemeji yake huyo kutaka kufunga ndoa tena wakati kikanisa hairuhusiwi.
Mhache, alisema walifikia hatua hiyo ya kwenda kanisani kusimamisha ndoa hiyo, kwa sababu Neema alikuwa bado ni mke wa mtu, hivyo hakustahili kuolewa na mwanamme mwingine na kwamba, aliondoka nyumbani akisema anakwenda kwa dada yake kupumzika.

0 comments:

Chapisha Maoni