Viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), jana waligoma
mbele ya Rais Jakaya Kikwete kuruhusu wajumbe wao kurejea katika Bunge
Maalumu la Katiba, walipokutana katika kikao cha kusaka suluhu ya mkwamo
wa mchakato wa Katiba.
Mkutano wa jana ulikuwa na sehemu mbili kuu, wa
kwanza ulifanyika katika Ikulu ya Kilimani, Dodoma ambako viongozi hao
walikutana na Rais Kikwete na mwingine katika Hoteli ya St. Gasper ambao
uliwashirikisha viongozi na maofisa wa vyama vilivyoshiriki bila Rais
Kikwete.
Mkutano huo ni matunda ya jitihada zinazofanywa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) ambacho kiliratibu mazungumzo hayo yaliyochukua zaidi ya saa mbili na nusu, katika Ikulu ya Kilimani, wakati yale ya St. Gaspar yalichukua takriban saa moja na nusu.
Mkutano huo ni matunda ya jitihada zinazofanywa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) ambacho kiliratibu mazungumzo hayo yaliyochukua zaidi ya saa mbili na nusu, katika Ikulu ya Kilimani, wakati yale ya St. Gaspar yalichukua takriban saa moja na nusu.
Viongozi walioshiriki kikao hicho cha Ikulu ni
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara), Philip Mangula, Katibu Mkuu wa
chama hicho, Abdulrahman Kinana, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod
Slaa na Mwanasheria wa chama hicho, Tundu Lissu, Mwenyekiti wa CUF,
Profesa Ibrahim Lipumba na Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Tanzania Bara),
Magdalena Sakaya.
Wengine ni Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James
Mbatia, Katibu Mkuu wake, Mosena Nyambabe, Mwenyekiti wa TLP, Augustine
Mrema, Mwenyekiti wa UDP ambaye pia ndiye mwenye zamu ya uenyekiti wa
TCD, John Cheyo na Mwenyekiti wa UPDP pamoja na mwakilishi wa vyama
visivyokuwa na wabunge ndani ya TCD, Fahmi Dovutwa.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho zinasema Rais
Kikwete baada ya kuanza kwa kikao hicho alitoa fursa kwa kila
aliyekuwapo kuzungumza na hapo zilijitokeza hoja mbalimbali, nyingi
mwelekeo wake ukiwa ni kutaka kusitishwa kwa Bunge Maalumu ili kutoa
fursa kwa nchi kuendelea na masuala mengine makubwa.
Chanzo chetu kilisema: “Rais amekuwa msikivu
kweli, amewasikiliza wote lakini ugumu ulianza kuonekana pale
ilipotolewa kauli ya kuwauliza wale watu wa Ukawa kama wanaonaje
wakirejea halafu hoja zao zikazungumzwa ndani ya Bunge Maalumu, yaani
hawataki kabisa kusikia hilo.”
Kuhusu hoja ya kusitishwa kwa Bunge, habari
zinasema ilijadiliwa kwa kirefu na wataalamu wa sheria wakijaribu kutoa
uzoefu wao, lakini kikwazo kilichoonekana ni Sheria ya Mabadiliko ya
Katiba ambayo haimpi Rais mamlaka ya kusitisha Bunge.
“Rais alisema hoja zao ni nzuri na zina mashiko,
lakini suala kubwa likawa ni kwamba tunafikaje huko wanakopendekeza?
Maana sheria iko kimya kuhusu mamlaka ya Rais kusitisha Bunge Maalumu,
ndiyo maana sasa tulitoka Ikulu tukaenda St. Gaspar ili kujadili, ngoja
tusubiri hiyo tarehe 8 maana siyo mbali,” alisema mmoja wa wajumbe wa
kikao hicho.
0 comments:
Chapisha Maoni