Alhamisi, Septemba 18, 2014

MAENEO YANAYOONGOZA KWA MAAMBUKIZI YA UKIMWI TANZANIA

Takwimu za tume ya kudhibiti ukimwi Tanzania (TACAIDS) zinaonyesha kuwa kiwango cha maambukizi ya Virusi vya Ukimwi katika barabara za kimataifa kwenye vituo vya kulaza magari ya mizigo ya masafa marefu kiko juu  ikilinganishwa na wastani wa taifa.
Wastani wa juu wa kitaifa wa maambukizi hayo unatajwa kuwa asilimia 5.1 wakati kwenye vituo hivyo ni kati ya asilimia 15 hadi 35.
Mratibu wa Program Maalumu ya TACAIDS Renatus Kihungo ameeleza Sababu zinazochangia ongezeko hilo na kueleza hatua wanazochukua kudhibiti hali hiyo kuwa ni pamoja na kuongeza vituo vya kutolea elimu katika barabara hizo ambavyo sasa vimefika 14.
Pamoja na mambo mengine ametaja baadhi ya huduma zitakazokuwa zikitolewa katika vituo hivyo kuwa ni pamoja na ugawaji wa kondom, huduma za ushauri nasaha, upimaji wa hiari, rufaa kwa matibabu maalumu, unasihi wa upimaji wa VVU na utoaji wa huduma ya habari elimu na mawasiliano.
Baadhi ya vituo hivyo ni Kagongwa- Kahama, Kibaigwa, Mdaula, Bagamoyo, Uvinza, Kasumulu Kyela na Tunduma Mbozi.

0 comments:

Chapisha Maoni