Justin Bieber ameshtakiwa kwa kushambulia mtu na kwa uendeshaji hatari
baada ya kugonga gari akiwa anaendesha pikipiki yake ya matairi manne.
Alikamatwa karibu na mji aliozaliwa wa Stratford, Ontario, baada ya
kuanza kupigana na dereva wa gari aliloligonga. Polisi wa Ontario
wamethibitisha kuwa waliitwa katika eneo la tukio kuchunguza na
wamekamata mtu. Polisi baadaye walimuachilia huru katika kile
kijulikanacho kama "ahadi ya kurudi tena" mahakamani Septemba 29. Kwa
mujibu wa taarifa ya polisi, uchunguzi "umeonesha kuwa baada ya ajali
hiyo kutokea, dereva wa gari na wa pikipiki 'walikunjana' mashati"
0 comments:
Chapisha Maoni