Jumanne, Septemba 30, 2014

HABARI ZA MATUKIO YA MAUAJI NA MADAWA YA KULEVYA IRINGA LEO

Mtu mmoja amefariki Mkoani Iringa kwa ajali ya barabarani huku jeshi la polisi likimshikilia mtu mmoja kwa tuhuma ya kukutwa na madawa ya kulevywa aina ya bhangi. Kamanda wa jeshi la polisi Mkoani Iringa ACP Ramadhani Mungi amesema Godfrey Nkini umri miaka 40 mkazi wa Dar es Saalam amefariki baada ya kutokea ajali ya kugongana kwa magari mawili ya mizigo maeneo ya Rungemba barabara kuu ya Iringa-Mbeya wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa. Kamanda Mungi ameongeza kuwa ajali hiyo imehusisha gari lenye namba za usajili T.135 BTD likiwa na tera namba T.347 BAS aina Scania lililokuwa likiendeshwa na marehemu akitokea nchini Congo kuelekea Dar es Salaam na kugongana na gari namba T.538 APP lenye tera namba T.605 BFM Aina ya Scania likiendeshwa na Charles Paison umri miaka 40 mkazi wa Mbeya. Aidha amesema ajali hiyo imepelekea majeruhi kwa Charles Paison na Thabiti Saleh umri miaka 30 mkazi wa Dar es Salaam ambao wamelazwa hospitari ya Mafinga wilaya ya  Mufindi Mkoa wa Iringa kwa matibabu zaidi chanzo chake kikiwa ni mwendo kasi. Hata hivyo Kamanda Mungi amesema askari polisi wakiwa doria maeneo ya Makorongoni Manispaa na Mkoa wa Iringa wamemkamata Zarina Juma umri miaka 25 mkazi wa mawelewele Manispaa ya Iringa akiwa na bhangi kete 68 alizozihifadhi kwenye mfuko wa suruali chanzo kikiwa ni kujipatia kipato.

0 comments:

Chapisha Maoni