Jumatano, Septemba 17, 2014

BOTI YAZAMA MTONI, WATU 80 WATOWEKA!

Wizara ya Uchukuzi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) imetangaza leo kuwa, kwa kiasi cha watu 80 hawajulikani walipo, baada ya boti waliyokuwa wamepanda kuzama katika Mto M'poko ulioko kusini mwa nchi hiyo. 
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Uchukuzi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati imeeleza kuwa, boti hiyo ilibeba zaidi ya watu 100, ambapo  watu 50 kati yao waliokolewa na wengine wasiopungua 80 hawajulikani walipo. Taarifa hiyo imeeleza kuwa, kuzama kwa boti katika Mto M'poko limekuwa jambo la kawaida, kwani vyombo hivyo vya baharini vinapakia watu na mizigo kupita kiasi.
Jamhuri ya Afrika ya Kati licha ya kuwa na utajiri mkubwa wa madini na ardhi ya kilimo, inakabiliwa na matatizo makubwa katika sekta ya miundombinu na lindi la umasikini.

0 comments:

Chapisha Maoni