Ijumaa, Agosti 15, 2014

MASANJA AELEZA MAONO YAKE JUU YA UCHUMBA WA DIAMOND NA WEMA

Kupitia kurasa yake ya mtandao wa Instagram Mchekeshaji Maarufu Afrika Mashariki pia ni Mtumishi wa Mungu Emmanuel Mgaya a.k.a Masanja Mkandamizaji ama waweza muita "Street Pastor" ameandika:
Street Pastor Anasema..Hili swala la diamond na wema nadhani mungu amemuhurumia mmoja wapo kati ya hao wawili. Kama wangekuwa watu wa kuoana wangesha oana uchumba gani mrefu kama wanasomea udokta???? Rafiki yangu nasib, kama kweli mlipendana kwa dhati hizo kasoro zinarekebishika, maana hakuna mwanadamu aliye sahihi kwan hata ww nasib unamapungufu yako. Na wewe dada yangu wema lazima ujue mme ndio kichwa cha nyumba kwa maelezo hayo inaonyesha haumsikilizagi mwenzio omba msamaha tenaaa na tena na ukubali kubadilika. Mi sipendi mkiwa mnaongozana wote kwenye ma show ya usiku mme kafanye kazi mke abaki home ukirudi mwili umepoa hata ujauzito unaingiaa!! Sasa woote stejini mkirudi miili ya moto si mtazaa popompoo jamaniii!! Nitafurahi kusikia tofauti zenu mmezimaliza kwa amani ili mashabiki wenu wasijisikie vibaya.

0 comments:

Chapisha Maoni