Jumanne, Julai 22, 2014

WANAWAKE WATAKA CHOMBO CHAO

UWEPO wa chombo maalum, umetajwa kama njia pekee ya kutatua kero za wanawake ambao kwa muda mrefu wamekandamizwa na mfumo dume, hivyo kubaki nyuma kiuchumi na kiuongozi.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala, Dk. Alexander Makulilo ndiye alitoa rai hiyo wakati akizungumza kwenye mjadala kuhusu mchakato wa katiba mpya.
Mjadala huo uliandaliwa na Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake na Watoto (WLAC) kwa msaada wa Shirika la kimataifa la OXFAM na kuwakutanisha wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini jijini Dar es Salaam.
Alisema kwa muda mrefu kumekuwa na fikra potofu, kwamba wanawake hawana uwezo ingawa kuna ushahidi wa wale ambao wamepewa nafasi na wamefanya vizuri.
Kwa mujibu wa mwanazuoni huyo, baadhi ya tafiti zilizofanywa mwaka 2013 na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kushirikiana na Taasisi ya Demokrasia (TCD), zimeonyesha kuwa wanawake wanachagulika iwapo watagombea nafasi mbalimbali za uongozi.

0 comments:

Chapisha Maoni