Jumatano, Julai 02, 2014

TETESI ZA USAJILI KATIKA MAGAZETI YA UINGEREZA

Liverpool inafikiria kumsajili mshambuliaji wa AC Milan Mario Balotelli, iwapo Luis Suarez atajiunga na Barcelona (Daily Express), Wakati huohuo Brendan Rodgers anamtaka beki Dejan Lovren kuwa mchezaji wa tatu kutoka Southampton kwenda Anfield, baada ya kumchukua Lambert na Lallana (Times), kiungo wa Colombia James Rodrigues anajiandaa kuondoka Monaco kwenda Real Madrid kwa pauni milioni 40, iwapo Real watamuuza Angel Di Maria (Daily Mail), Arsenal watathibitisha kumsajili Mathew Debuchy kutoka Newcastle baada ya Kombe la Dunia (Daily Star), mshambuliaji wa Porto Jackson Martinez amekiri kuwa angependa kujiunga na Arsenal, klabu ambayo alikuwa akiishabikia akiwa mtoto (Daily Express), Manchester City wamekubaliana na Roma kumsajili beki wa kati Mehdi Benatia, lakini watasubiri Roma wapate mtu wa kuziba pengo (Daily Mirror), kipa wa Costa Rica Keylor Navas anajiandaa kuhamia England baada ya Arsenal nao kujiunga na Liverpool kumsaka (Daily Star), Manchester United watatoa pauni milioni 20 kumsaka beki wa Borussia Dortmund Mats Hummels wiki hii (Metro). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa.

0 comments:

Chapisha Maoni