Jumatano, Julai 23, 2014

ROMA ATIMIZA AHADI BAADA YA BRAZIL KUFUNGWA, SASA AFANTA KAZI NA BOB JUNIOR

Hitmaker wa Mathematics Roma Mkatoliki ametmiza ahadi yake ya kwenda kufanya wimbo katika studio za Sharobaro Records chini ya producer Bob Junior aliyoweka wakati wa kombe la dunia kama Brazil ingefungwa na Ujerumani. Katika studio hiyo, Roma amerekodi wimbo uitwao ‘Maumivu’.  
Bob Junior amesema amefurahishwa na uamuzi wa Roma wa kumuamini na kuanza kufanya kazi hiyo ambayo itatoka wiki ijayo.
Roma jana alikuwa kwangu na tumeandaa ngoma mpya inaitwa Maumivu na itatoka next week
amesema Bob Junior.
Nashukuru ameweza kuelewa kuwa nina kitu gani, kaja hapa hakuamini alichokisikia kwa sababu nilimwambia nafanya Hip Hop nzuri sana lakini hakuniamini lakini jana kaja nafikiri alifika saa 4 akaondoka saa kumi asubuhi, yaani saa kumi alfajiri. Tumefanya kazi tumeishia nusu lakini tutaimalizia leo, lakini next week itatoka hii collaboration.
Katika account yake ya Instagram Roma alipost picha hii kama ahadi...

0 comments:

Chapisha Maoni