Jumanne, Julai 08, 2014

POLISI YATOA TAMKO JUU YA MATUKIO YA MABOMU

Kufuatia kushamiri kwa matukio ya watu kufanya matukio ya uhalifu kwa kutumia mabomu jeshi la polisi limesema  litahakikisha linauteketeza mtandao wa watu hao wanaojihusisha na  vitendo hivyo ambapo mpaka sasa zaidi ya watu 25 wanashikiliwa kwa nchi  nzima kutokana na kujihusisha na matukio hayo.
Kufuatia kushamiri kwa matukio ya watu kufanya matukio ya uhalifu kwa kutumia mabomu jeshi la polisi limesema  litahakisha linauteketeza mtandao wa watu hao wanaojihusisha na  vitendo hivyo ambapo mpaka sasa zaidi ya watu 25 wanashikiliwa kwa nchi nzima kutokana na kujihusisha na matukio hayo.
Akizungumza jijini dar es salaam mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai isaya mngulu amesema siyo kwamba jeshi la polisi limeshindwa kupambana na matukio hayo ila kazi bado inaendelea japo wananchi wanapaswa kutoa taarifa kwa kila jambo wanaloona halipo sawa.
Chanzo kilitembelea katika taasisi ya mifupa moi na kufanikiwa kuzungumza na msemaji wa taasisi hiyo bw almas juma kuhusu  hali ya majerui  wawili waliolazwa katika hosptal hiyo wakitokea Arusha kufuatia kulipuliwa kwa bomu wakiwa katika futari  amesema ali zao  zinaendele vyema.
Aidha ilifanikiwa kuzungumza na  majeruhi hao sheikh Soud  Ally Soud  na  sheikh Muhaji Hussein  ambao wanaelezea hali ilivyo kuwa huku wakiliomba jeshi la polisi kulishughulikia kwa kina jambo hilo.

0 comments:

Chapisha Maoni