Jumatano, Julai 23, 2014

BWENI LAUNGUA MONDULI, ARUSHA, LOWASA AHUSIKA KWA 100%

Kiasi cha wanafunzi 100 wa shule ya sekondari ya Erikisongo wilayani Monduli wamenusurika kifo baada ya vyumba vitano vya mabweni yao kuteketea na moto leo(Jumatano) asubuhi.
Moto huo ambao inaelezwa chanzo chake ni hitilafu ya umeme ilitokea wakati wanafunzi wote wako darasani. Hakuna mtu yoyote aliyedhurika lakini mali kadhaa za wanafunzi zimeteketea.
Kikosi Cha zimamoto kutoka Arusha kulifikisha wakati tayari mabweni hayo yameshateketea.

Edward Lowasa kama Mbunge wa Monduli ametembelea shule hiyo na kuwaahidi kuwasafirisha wanafunzi majumbani kwao wakati utaratibu unafanywa kurejesha katika hali ya kawaida. Gharama za kuwasafirisha ni shilingi laki Saba.
Aidha Lowasa kama mbunge wa Monduli kwa kushirikiana na kiwanda Cha magodoro Cha Tanform Cha Arusha kimetoa msaada wa magodoro 100 kufuatia kadhia hiyo.

0 comments:

Chapisha Maoni