Jumamosi, Juni 14, 2014

VIONGOZI WA CHADEMA MASASI WASHINDA KESI DHIDI YA SERIKALI NA KUACHIWA HURU MTWARA

MAHAKAMA ya Wilaya ya Masasi, mkoani Mtwara, jana imewaachia huru viongozi watatu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), pamoja na washitakiwa wengine 21 waliokuwa wakikabiliwa na kesi tatu tofauti za kufanya maandamano bila kibali.

Hakimu mkazi wa mahakama hiyo, Halfani Ulaya, aliwaachia huru viongozi hao ambao ni Kaimu Mwenyekiti wa Mkoa, Kasim Ahmad Bingwe, Katibu wa Wilaya, Fidelis Vitus Mlaponi na Katibu wa Jimbo, Musa Mustafa Mwadewa pamoja na washitakiwa wengine 13 ambao aliwaona hawana hatia katika kesi namba 263 ya 2013.
Akizungumza na Fichuo TZ baada ya kesi hiyo jana, wakili aliyepelekwa Masasi na CHADEMA ili kuwatetea viongozi hao, Nyaronyo Mwita Kicheere, alisema Bingwe, Mlaponi na Mwadewa pamoja na wenzao 13 walikuwa wanakabiliwa na makosa ya kuandamana bila kibali, kuchoma moto nyumba na kuharibu mali ya Mbunge wa Masasi, Mariamu Kasembe (CCM).

0 comments:

Chapisha Maoni