Alhamisi, Juni 12, 2014

MFAHAMU KASA ALIYETABIRI KUWA BRAZIL INASHINDA DHIDI CROATIA LEO KATIKA MECHI ZA UFUNGUZI KATIKA FIFA 2014

BAADA ya pweza Paul aliyekuwa akiishi Ujerumani kujizolea umaarufu wakati wa Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010 nchini Afrika Kusini, fainali za mwaka huu nchini Brazil ameibuka mtabiri mwingine aitwaye Cabeção au Big Head.
Big Head ambaye ni kasa mwenye umri wa miaka 25, anayeishi katika kijiji cha Praia Do Forte nchini Brazil ameitabiria nchi yake ya Brazil kuibuka na ushindi katika mechi ya ufunguzi kwenye Fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Croatia kesho.
Big Head ameanza kazi yake hiyo jana, Jumanne kwa kutabiri mechi ya ufunguzi kati ya Brazil na Croatia. Kasa huyo anafanya utabiri kwa kuchagua vyakula. Alichagua mmoja wa samaki waliokuwa wananing'inia katika bendera za Brazil, Croatia na kwenye mpira.

0 comments:

Chapisha Maoni