Jumapili, Juni 08, 2014

HOMA YA UCHAGUZI 2015, HIVI NDIVYO WANASIASA WANAVYOWINDWA

HOFU ya siasa za kuchafuana kuelekea katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani imeanza kushika kasi miongoni mwa wabunge ambao tayari wameanza kuanikwa picha zao kwenye mitandao ya kijamii wakiwa faragha.
Fichuo TZ imedokezwa kuwa baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakifadhili upigaji wa picha za video na mnato kwa kuwatumia wahudumu wa hoteli mbalimbali za ndani na nje ya Mkoa wa Dodoma, kunakofanyika vikao vya Bunge.
Inaelezwa kuwa lengo la kufadhili mikakati hiyo ni kuwaharibia majina wabunge husika ili wasipate fursa ya kuaminika kwenye jamii, hivyo kunyimwa kura katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu mwakani.
Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa kuwa kutokana na kukua kwa teknolojia ya habari na mawasiliano, baadhi ya wataalamu wa masuala ya mitandao wamekuwa wakitengeneza picha za ngono kwa lengo la kujipatia fedha kwa njia zisizo halali.
Inadaiwa baadhi ya watu huwasiliana na wahusika juu ya picha hizo huku wakiwatishia kuwa endapo wasipowapa fedha watazitoa kwenye jamii.
Tayari picha za Mbunge wa Mbinga Magharibi, John Komba (CCM) na Ukerewe, Salvatory Macheli (CHADEMA), zimetolewa zikiwaonyesha wakiwa faragha.
Komba, alikaririwa na vyombo vya habari kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakitumia teknolojia kutengeneza picha hizo kwa malengo ya uovu.

0 comments:

Chapisha Maoni