Jumapili, Juni 15, 2014

FIFA 2014 BRAZIL: VAN GAAL ATOBOA SIRI KUBWA YA USHINDI WA UHOLANZI DHIDI YA HISPANIA

Van Gaal amefunguka kwamba aliruhusu wake na ma-girl friends kuwatembelea wachezaji wa timu ya taifa ya Uholanzi katika maandalizi ya mchezo wao mgumu dhidi ya mabingwa watetezi wa Kombe la Dunia - Spain.
Alisema:
Misimamo yangu ni masuala yote. Ubinadam, mchezaji.
Akili ya mchezaji na fikra husaidiana kujenga utulivu. Na fikra hujengwa na mazingira yanayomzunguka mchezaji.
Kwa hiyo siku ya Alhamisi na asubuhi kabla ya mchezo nilitoa ruhusa kwa wake na marafikiki zao wa kike lengo likiwa ni kuwafurahisha na wawe na furaha.
Nilishawaambia wachezaji kwamba kuna wakati nitakua naruhusu wake na watu wao wa karibu kuwatembelea kambini
Matokeo ya kuwapa utulivu wachezaji kambini kabla ya mchezo na kuwapunguzia msongo wa mawazo (mbinu ya van Gaal) ni historia katika soka, kwani wameweza kuifunga timu ngumu ya Spain na watetezi wa kombe hili la Dunia jumla ya bao 5-1 na zingeweza kufika hata 8.
Nini maoni yako? unadhani hii mbinu ni nzuri ama inaweza ua kabisa stamina kwa wachezaji wasio na nidhamu ya jambo

0 comments:

Chapisha Maoni