Jumamosi, Juni 07, 2014

DIAMOND APIGIWA MAGOTI NA CHANNEL O

Katika hali isiyo ya kawaida Diamond Platnumz azidi kutokewa na bahati kila siku, ila kwa hili si bahati tu,ila ni zaidi ya bahati cause haijawahi kutoke kwa mwanamuziki yeyote mwingine hapa east africa. Story nzim ilikuwa hivi;Mapema alhamisi ya wiki hii Diamond platnumz alikutana na manager wa televisheni ya kimataifa ya Channel O, Diamond akiwa anahojiwa na kipindi kimoja cha redio alizidi kufunguka zaidi na kusema , alipokutana na manager huyo, alipata nafasi ya kumuonyesha video yake mpya aliyoifanya huko uingereza, ile kuiona tu hakuamini kuwa kuna vitu adimu kama hivi huku east africa, na kumuomba Diamond hapo hapo aweze kumpa uwezo wa kuicheza exclusive (kwa mara ya kwanza) video hiyo Channel O, Diamond aliona kama utani hivi ila bada ya kuongea na producer wa video hiyo, ambaye ndiye aliyeitengeneza video yake ya my number one remix aitwaye Clarence, alimpa meneja huyo wa Channel O na baada ya muda, alishtuka kuona watu wakimtumia ujumbe kumpa hongera kutokana na video hiyo jinsi ilivyo kali baada ya kupigwa Channel O.

Ilikuwa tuitoe officialy kwenye media baada ya tuzo hizi kuisha na tulisubiri muda mzuri wa kuachia video hiyo, ila imetokea kama bahati ya kuombwa video hiyo kupigwa exclusive katika channel O, cause walisema lete tuipige kipindi hiki, tuonyeshe vipaji vilivyotoko east africa, na nashukuru kwa hilo, ila naona officialy hivi karibuni itabidi niitoe pamoja na nyimbo yake
alimalizia Diamond Platnumz ambaye kwa hivi sasa yupo huko jijini Durban, katika matayarisho ya Tuzo za Mtv MAMA

0 comments:

Chapisha Maoni