Alhamisi, Mei 29, 2014

WAKAZI WA KIGAMBONI KULIPWA MPAKA TSH.MILIONI 141 KAMA FIDIA YA VIWANJA

WATU walio kwenye eneo la mradi wa uendelezaji wa Mji Mpya wa Kigamboni jijini Dar es Salaam, wamepangiwa viwango vya fidia ya Sh milioni 141 kwa ekari katika awamu ya kwanza.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka alisema hayo juzi usiku wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2014/15.
Wakazi wa eneo hilo, wameshauriwa kuendelea kuwa wavumilivu na kutokubali kurubuniwa kwa kuuza maeneo yao kwa wajanja, ambao inaelezwa baada ya viwango vya fidia kutajwa, wamejitokeza wakitaka kununua ardhi kwa bei poa, baadaye wafidiwe.

0 comments:

Chapisha Maoni