Jumatatu, Mei 26, 2014

UCHAGUZI WA MALAWI NI MIZENGWE TU

Uchaguzi mkuu wa Malawi umeendelea kubeba sura mpya ya sarakasi za mapingamizi ya kisheria, baada ya mahakama kuu ya Lilongwe kuamuru Tume ya uchaguzi nchini humo iendelee na mipango ya kazi zake bila kuingiliwa na mamlaka yeyote.
Uamuzi huo umetokana na ombi la chama cha Malawi Congress MCP kutaka mahakama hiyo izuwie amri ya Mahakama kuu ya Blantyre iliyo iamuru tume ya uchaguzi kuhesabu kura na kumtangaza mshindi ndani ya siku 8, likiwa ni ombi la chama cha DPP.
Mwandishi wa BBC Baruan Muhuza aliye mjini Lilongwe anasema kuwa uamuzi huo sasa una maana kwamba MCP imeshinda kesi ambapo pamoja na mambo mengine wanataka kazi ya kuhesabu kura ianze upya nchi nzima jambo ambalo ndiyo maamuzi ya tume na vyama vyote vya siasa isipokuwa DPP.
Tume ya uchaguzi inakutana mjini Blantyre na itatoa taarifa baadaye kuhusu uamuzi uliochukuliwa na Mahakama Kuu hii leo.
Huku ikijulikana wazi kuwa kinachosubiriwa sasa ni ama kurudiwa kuhesabu kura za maeneo yenye mgogoro au kura zote za nchi nzima.

0 comments:

Chapisha Maoni