Msanii chipukizi wa Bongo Fleva, Venas John Bebu ‘Bebuz’ amenaswa laivu
akivunja amri ya sita (kuzini) na mwanafunzi wa sekondari ufukweni.
Tukio hilo la aibu lilijiri wiki iliyopita mishale ya saa 8:00 usiku
kwenye Ufukwe wa Coco, Dar ambapo polisi jamii walimnasa jamaa huyo
aliyedaiwa ni swahiba mkubwa wa mwanamuziki, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’
ambao hivi karibuni walitoa kibao kipya kijulikanacho kwa jina la
Bunyerobunyero.
Mara baada ya kunaswa, Bebuz alianzisha varangati kubwa lakini polisi
jamii walimtuliza kwa virungu kisha kumfunga pingu na kumtaka atulize
mzuka atoe ushirikiano vinginevyo angeumia.
Ufukwe wa Coco umekuwa ukilalamikiwa kwamba hukutanisha watu wenye
malengo mbalimbali lakini wanaokwenda kwa ajili ya kufanya ufuska usiku
ni wengi hasa siku za wikiendi ambako kunakuwa na burudani ya disko.
Katika siku za hivi karibu, machangudoa wamekuwa wengi ufukweni hapo na
baadhi yao ni vibaka ambao wamekuwa wakitoka nduki na nguo za wanaume
huku wakisachi na kuchukua kila kitu.
0 comments:
Chapisha Maoni