Jumapili, Mei 18, 2014

ISABELA MPANDA AACHA NYETI ZAKE KWEUPE! NI KATIKA KITCHEN PARTY

Miss Ruvuma 2006, Isabela Mpanda amedhihirisha jinsi alivyo hamnazo baada ya kuvua nguo hadharani na kuacha nyeti nje bila kujali watu waliokuwa wakimshangaa.
Tukio hilo la kushangaza lilitokea Alhamisi iliyopita kwenye Ukumbi wa Mawela uliopo Sinza, Dar ambako kulikuwa na kitchen party ya mwigizaji, Vanita Omary ambapo Isabela aliwashangaza watu baada ya kuacha nyeti nje.

Bila chembe ya aibu, Isabela akivalia gauni fupi akiwa tilalila, alikuwa akicheza muziki huku akilinyanyua gauni juu na kuacha sehemu nyeti za makalio nje na kusababisha ‘kufuli’ yenye muundo wa bikini kuonekana.
Ishu hiyo ilizua minong’ono kwa baadhi ya wageni waalikwa na kubaki wakimshangaa kwa kitendo hicho na kudai kuwa ni hamnazo.
Akiwa anafanya tukio hilo la kujifunua alisikika akisema amepania sherehe hiyo kwani yeye ndiye wifi wa Vanita na kama mwigizaji Jacqueline Wolper aliacha kufuli lake kubwa wazi na yeye aliamua kuonyesha lake aina ya bikini nje ili lionekane kwani ni la bei kubwa.

Mh, kweli huyu Isabela hamnazo yaani anajifunua mbele za watu, hata haogopi, ukweli anatia aibu lakini afadhali wanaume hawapo maana wangekuwepo ingekuwa aibu zaidi
 walisikika wasanii wawili wakijadiliana huku wakimkodolea macho mwanadada huyo.

0 comments:

Chapisha Maoni