Jumanne, Mei 27, 2014

HATARI SANA HII KUHUSU LAP TOPS NA SMART PHONES

Miongoni mwa changamoto kubwa iliyopo sasa katika nchi zilizoendelea na zinazoendelea kwa watumiaji wa simu za mikononi ni kupotewa na simu zao ama kuibwa.
Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 56 ya watumiaji wa vifaa vya mawasiliano duniani hupoteza simu na kompyuta mpakato kila mwezi. Nchini Marekani pekee kila baada ya dakika moja simu 113 hupotea ama kuibwa.
Wakati tatizo la wizi wa simu na tabiti likiendelea, watengenezaji wa vifaa hivyo hawako nyuma, nao sasa wanabuni teknolojia zinazomwezesha mmiliki kukipata kifaa chake kilichopotea au kuibwa.

0 comments:

Chapisha Maoni