Alhamisi, Mei 22, 2014

DIAMOND TENA! SASA NI KATIKA TUZO ZA AFRIMMA 2014, ANASHINDANA KATIKA VIPENGELE VITANO...YUPO PIA BEN POL, MRISHO MPOTO NA SHEDDY CLEVER

Diamond, Ben Pol, Sheddy Clever na Mrisho Mpoto wametajwa kuwania tuzo za Africa Music Magazine Awards , AFRIMMA 2014.
Diamond ndiye aliyetajwa kwenye vipengele vingi zaidi (5) vikiwemo Msanii wa mwaka, Wimbo wa mwaka, Collabo bora, Video bora ya mwaka na Msanii bora wa kiume wa Afrika Mashariki.

Ben Pol ametajwa kuwania tuzo ya Msanii bora wa kiume wa Afrika Mashariki, Sheddy akitajwa kuwania kipengele cha mtayarishaji bora wa mwaka na Mrisho Mpoto akitajwa kuwania kipengele cha Msanii bora wa muziki wa asili.

0 comments:

Chapisha Maoni