Jumatatu, Machi 05, 2018

75% YA WANAOACHA KAZI HUACHA SABABU YA 'MABOSS' WAO

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na watafiti kutoka shirika la kazi ulimwenguni ILO imebainika kuwa asilimia kubwa ya waajiriwa wanaoziacha kazi zao walikoajiriwa huacha kazi huwa sababu halisi ni 'maboss' wao.
Tunaambiwa kuwa 75% ya waajiriwa anaojiuzulu nafasi zao katika ajira ni wale wenye matatizo mbalimbali na viongozi wao kwenye mashirika, na 25% inayosalia pekee ni wale wanaoacha kazi zao kwa sababu nyinginezo.
Mashirika mengi kutokana na ukubwa wake au majina yaliyokuzwa na huduma zitolewazo hapo huvutia watu wengi kutaka kufanya kazi ndani yake lakini punde wajiungapo na mashirika yenyewe hukutana na visanga vya 'maboss' wao. Sasa kumbe kuna mambo mawili hapa, suala la kupata ajira ni moja na kupata viongozi wazuri ni sababu nyingine.
Lakini hili linatuonesha mambo mawili makubwa; Kwanza inaonesha dhahiri kuwa viongozi ndiyo huharibu picha nzuri ya taasisi na ni hao hao hufanya mahala pa kazi pasiwe salama kwa wafanya kazi.

1 comments: