Jumatatu, Mei 26, 2014

BILIONEA ASHINDA KITI CHA URAIS UKRAINE

Matokeo ya kura yaliotangazwa nchini Ukraine yanaonyesha kuwa Tajiri Petro Poroshenko ameshinda awamu ya kwanza ya uchaguzi wa urais nchini.
Matokeo hayo yanaonyesha kuwa Poroshenko amepata asilimia 55 huku mpinzani wake wa karibu Yulia Tymoshenko akipata asilimia 13.Bi Tymoshenko amekubali kushindwa.
Huku akitangaza ushindi wake baada ya shughuli ya kuhesabu kura kukamila,Petro Poroshenko amesema kuwa ziara yake ya kwanza baada ya kutawazwa kama rais itakuwa katika eneo la Donbas mashariki mwa taifa hilo ambapo wanaharakati waliojihami wametangaza uhuru wao.
Amesema kuwa atawasemehe watu wanaomiliki silaha,lakini sio wale wanaowauwa raia.

0 comments:

Chapisha Maoni