Alhamisi, Aprili 17, 2014

RAIS KIKWETE: SIO ADABU KUWATUKANA HAYATI NYERERE NA MZEE KARUME

Rais Jakaya Kikwete, amesema kuwa ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa adabu, kwa baadhi ya Watanzania kuwatukana, kuwadhihaki na kuwakejeli Waanzilishi wa Taifa la Tanzania, Hayati Julius Nyerere na Hayati Sheikh Abeid Amaan Karume.
Rais Kikwete amesema kuwa viongozi hao wawili wameifanyia Tanzania mambo mengi makubwa na ya kihistoria, kiasi cha kwamba Watanzania wanao wajibu wa kudumisha na kuenzi heshima yao kwa namna ya kudumu.
Rais Kikwete ametoa msimamo huo baada ya kuwa ameulizwa kuhusu matusi, kejeli, dhihaki ambazo zimekuwa zinaonyeshwa na wajumbe wachache wa Bunge Maalum la Katiba juu ya waasisi hao wa Tanzania na Wabunifu Wakuu wa Muungano wa Tanzania.

0 comments:

Chapisha Maoni