Jumatano, Aprili 16, 2014

MERSON: LAZIMA ARSENAL ISHINDE ILI WAKAE NNE BORA


Klabu ya Arsenal ilikuwa lazima iifunge Wigan kwa penati lakini walishindwa kuonyesha nia kutokana na jinsi walivyocheza licha ya kushinda katika mchezo huo wa nusu fainali ya kombe la FA.
Mchambuzi mahiri wa soka,Paul Merson anakiri kuwa Arsenal walikuwa na bahati sana kuifunga timu hiyo ya Championship na anasema yalikuwa matokeo makubwa sana kwa kikosi hicho cha Arsene Wenger kutinga fainali.
Lakini akasisitiza,”Kama wanataka kuingia katika nne bora,wanahitaji kujifunza kutoka hapa kwasababu kama wanacheza kwa jinsi walivyocheza Jumamosi mpaka mwisho wa msimu basi hawawezi kupata nafasi ya kushiriki ligi ya mabingwa barani Ulaya.”
Huku akisema majeruhi hayajawasaidia kwani wachezaji kama Aaron Ramsey na Theo Walcott hawawezi kuwa wachezaji wa kiwango cha dunia lakini ni wachezaji muhimu na hodari zaidi kwa Arsenal.

Na kuongeza kuwa bila Theo wamekuwa wakipata tabu sana wakati Wenger amekuwa akiwatumia chipukizi,Yaya Sanogo mbele ya Olivier Giroud lakini haijasaidia kitu katika timu.
 Merson akasisitiza kuwa mfaransa huyo inabidi abadilishe hiyo staili pindi atakapocheza na West Ham na kumchezesha kiungo mmoja mshambuliaji kwasababu vijana wa Sam Allardyce wataenda Emirates Stadium kupaki basi.
Pia akasema alipoangalia ratiba alihisi mchezo huo utakuwa mgumu sana hivyo akakiri kuwa Arsenal wanapaswa kucheza kwa kujiamini,kujituma na kutafuta magoli ya mapema zaidi.
Mwisho akasema kuwa mchezo huo Arsenal wanaenda na kushinda 2-0.

0 comments:

Chapisha Maoni