Jumatatu, Machi 17, 2014

WANAWAKE WASHIKILIWA NA POLISI BAADA YA KUMKOSEA ADABU WAZIRI MKUU

Polisi nchini Uturuki wamewazuilia wanawake wawili waliomfanya ishara mbaya ya mkono waziri mkuu wa nchi hiyo Recep Tayyip Erdogan wakati wa maandamano ya kupinga serikali.
Waziri mkuu alisikika akilalamika kuwa wanawake wawili walimfanyia ishara inayodhihirisha utovu wa nidhamu wakati wa maandamano na mkutano wa hadhara.
Hatua ya kuwazuilia wanawake hao inakuja baada ya bwana Erdogan kumkaripia mmoja wao aliyemfanyia ishara chafu ya mkono alipokuwa akielekea kuhudhuria mkutano wa kisiasa Magharibi mwa nchi hiyo.
Waziri mkuu inasemekana alighadhabishwa mno kwa kuwa waliomfanyia ishara hiyo walikuwa wanawake wala sio wanaume.
''Ningeweza kuelewa ikiwa kitendo hiki kilifanywa na mwanamume, lakini badala yake kimetoka kwa mwanamke , ni vibaya sana,'' alinukuliwa akisema bwana Erdogan.
Waziri mkuu huyo amekuwa akikabiliwa na upinzani mkali tangu kuibuka kwa kashfa ya ufisadi dhidi yake Disemba mwaka jana ikiwahusisha washirika wake na kumsababishia changmoto kubwa katika uongozi wake kwa miaka 12 huku uchaguzi ukitarajiwa Machi tarehe 30.

0 comments:

Chapisha Maoni