Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia
misaada ya kibinadamu ameelezea hali mbaya inayowakabili wananchi wa
Sudan Kusini.
Valerie Amos ambaye mwezi uliopita alifanya safari nchini Sudan
Kusini ameeleza kuwa, licha ya kufikiwa makubaliano ya usitishaji
mapigano kati ya majeshi ya serikali na waasi nchini humo, maisha ya
mamilioni ya wananchi wa nchi hiyo yamo hatarini kutokana na kuendelea
mapigano ya hapa na pale, ukosefu wa chakula na kuibuka maradhi ya
milipuko nchini humo.
Valerie Amos ameongeza kuwa, zaidi ya watu 100
wameuawa wakiwa mahospitalini au makanisani ambako walikwenda kutafuta
hifadhi. Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, kambi za
wakimbizi za Umoja wa Mataifa zinawahifadhi wakimbizi wasiopungua elfu
ishirini, na kusisitiza kuwa zaidi ya watu laki tisa wameyakimbia makazi
yao na wengine laki moja na elfu tisini wamelazimika kukimbilia nchi
jirani.




0 comments:
Chapisha Maoni