Hivi karibuni Ommy Dimpoz alishoot video ya wimbo wake mpya jijini
London Uingereza na muongozaji maarufu barani Afrika na Ulaya, Moe Musa
ambaye ameshoot video za mastaa kibao zikiwemo Antenna na Azonto za Fuse
ODG, Caro ya Wizkid na Skelewu ya Davido.
Model atakayeonekana kwenye video hiyo ni maarufu sana jijini London aitwaye Sofia Skvortsova. Sofia Skvortsova
alizaliwa na kukulia Riga, Latvia. Ana asili ya Urusi, Ujerumani na
Poland.
Kazi yake ya umodel hufanyia jijini London hufanya kazi na mawakala wa mamodel. Amekuwa akifanya shughuli hiyo kwa zaidi ya miaka mitano barani Ulaya na Mashariki ya Kati.
Ameshaonekana kwenye majarida kibao, filamu, matangazo na video za muziki.





0 comments:
Chapisha Maoni